#Mungu

Active
136quotes

Quotes about mungu

Mungu, a Swahili term for God, embodies the essence of divine presence and spiritual connection. It represents a profound concept that transcends cultural and religious boundaries, offering a universal symbol of hope, faith, and guidance. In many African cultures, Mungu is not just a deity but a source of inspiration and strength, a beacon that illuminates the path through life's challenges. People are drawn to quotes about Mungu because they encapsulate the timeless wisdom and comfort that faith in a higher power can provide. These quotes often serve as reminders of the resilience and courage that can be found in spirituality, encouraging individuals to seek solace and understanding in the face of adversity. The allure of Mungu lies in its ability to evoke a sense of peace and purpose, fostering a deeper connection to the world and to oneself. Whether one is seeking motivation, reassurance, or a moment of reflection, quotes about Mungu offer a rich tapestry of insights that resonate with the human spirit, inviting contemplation and a renewed sense of hope.

"
Ukiwa karibu na Mungu utakuwa na maarifa kuliko profesa, Mungu ana maarifa kuliko profesa.
"
Tovuti za miadi (‘dating sites’) hutumia ‘optimal stopping’ kuwachagulia watu wachumba wao. Wanachofanya ni kwamba wanachagua watu 100. Wanaondoa 37% ya kwanza ya wale ambao sifa zao haziendani na sifa unazozitaka. Kisha wanakuchagulia mtu waliyeona ni bora zaidi kuliko wote waliobakia. Huyo waliyekuchagulia anaweza kuwa mke au mume bora. Lakini Mungu ana mipango yake. Unaweza kushangaa mke au mume bora akatoka kwenye 37% ya wale walioachwa.
"
Ukitaka Mungu akukumbuke jisahau!
"
Ukimtafakari sana Mungu utamwona.
"
Mungu anajibu kwa ghafla!
"
Heshimu kila mtu. Ongea na kila mtu. Msikilize kwa makini kila unayeongea naye. Maana Mungu anaweza kumtumia mtu yeyote, hata kichaa, kukupa ufunuo wa mambo yake.
"
Mungu anataka tujifunike kwa ngao yake. Yaani, tuwe na imani iliyokomaa katika Bwana na yeye atatufunika. Maana ya kauli hiyo ni kwamba kila kiungo cha miili yetu kuanzia unyayo hadi kichwa lazima kifunikwe kwa silaha ya Mungu, ambayo Mungu anaiita panoplia. Panoplia haimo katika kamusi ya Kiswahili au Kiingereza, lakini maana yake ni ‘ngao kamili ya Mungu’. Hii si tu silaha ya Mungu. Ni silaha kamili ya Mungu tunayotakiwa kujifunika kwayo.
"
Kama miaka 1000 ya duniani ni sawa na siku moja ya Mungu; hivyo basi, miaka 930 aliyoishi Adamu ni sawa na siku 0.93 au saa 22:32 za Mungu. Kwa hiyo, ili siku ya Mungu itimie Adamu alipaswa kuishi miaka 70 (siku 0.07 au saa 1:68) zaidi! Ukiidadavua saa 1:68 unapata saa 2:08. Kulingana na muda wa mbinguni tunapaswa kuishi kwa muda wa saa 2:08! Muda huo ni mfupi sana.
"
Adamu ndiye mtu wa kwanza kumjua Mungu.
"
Shetani ni mungu wa dunia hii kwa wale wasiomwamini Mungu. Kwa wale wanaomwamini Mungu, Mungu ndiye Mungu wa dunia hii.
Showing 1 to 10 of 136 results